1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 22 wauawa mashambulizi mji wa Rafah, Ukanda wa Gaza

29 Aprili 2024

Mashambulizi ya anga ya Israel katika mji wa Rafah kusini mwa Gaza yamesababisha vifo vya takriban watu 22, ikiwa ni pamoja na wanawake sita na watoto watano.

https://p.dw.com/p/4fI8S
Ukanda wa Gaza | Mji wa Rafah
Mamia kwa maelfu ya Wapalestina wamekwama kwenye mji wa Rafah, ambao Israel imesema inalenga kuushambulia. Picha: Haitam Imad/EPA

Kulingana na maafisa wa afya wa Wapalestina mmoja wa watoto waliouawa katika mashambulizi hayo ya usiku wa kuamkia leo alikuwa wa siku 5 tu.

Msemaji wa Ikulu ya Marekani John Kirby amesema juhudi za kufikia makubaliano ya usitishaji vita kati ya Israel na kundi la Hamas kwa wiki sita bado yanaendelea.

Haya yanajiri huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken akianza ziara yake ya saba katika Mashariki ya Kati tangu vita vya Israel na Hamas kuanza zaidi ya miezi sita iliyopita.